Radio Fadhila
Radio Fadhila
10 May 2025, 8:51 AM

Mratibu wa mradi Bridge Tanzania kitaifa Bi Fatma Shabani Mrope. Picha na Google
mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano katika wilaya tatu ambazo ni Masasi, Geita na Kaskazini Unguja, pia unawapa nafasi hawa Vijana na haswa Wanawake ni kwa asilimia 55% na Wanaume asilimia 45%
Na Neema Nandonde
Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya UNESCO ya Nchini Korea – Korea National Commission for UNESCO (KNC- UNESCO), inatarajia kutekeleza Mradi wa Bridge Tanzania unaolenga kuwainua vijana ambao wamekosa kuingia kwenye mfumo rasmi wa elimu na wanaishi katika mazingira magumu ili kuwainua kiuchumi.
Akizungumza na redio Fadhila May 8, 2025 Mratibu wa mradi huo kitaifa Bi Fatma Shabani Mrope amesema, mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano katika wilaya tatu ambazo ni Masasi, Geita na Kaskazini Unguja, pia unawapa nafasi hawa Vijana na haswa Wanawake ni kwa asilimia 55% na Wanaume asilimia 45%.
Amefafanua kuwa mradi huo unatarajiwa kuwafikia vijana 1,000 kutoka kila wilaya, huku miongoni mwa vigezo ikiwa ni pamoja na kijana kuwa na umri wa kuanzia miaka 16 hadi 30.
Amesisitiza kuwa, kwa kushirikiana na wilaya lengwa, wataangalia namna ya kupata vigezo rahisi vya kuwapata vijana hao ili kusiwe na ugumu wa vijana kuitumia apasavyo fursa hiyo.
Ameongeza kuwa Shirika kwa Kushirikiana na Halmashauri itahakikisha Vijana wanatambulika na hatimaye kuwakutanisha na Wataalamu mbalimbali na kuwapatia maarifa stahiki kupitia Mradi huo yatakayowawezesha Vijana kuanzisha Miradi ya Kiuchumi.
Sauti ya 1 ya Mratibu wa mradi Bridge Tanzania kitaifa Bi Fatma Shabani Mrope.
Aidha Bi. Fatma amewataka vijana kujitokeza kwenye mradi huo, kwakuwa watakaopata nafasi hiyo, muda wa mafunzo hautaathiri shughuli zao nyingine wanazozifanya , huku akisisitiza kuwa wakati wa mafunzo watawezeshwa na tume kupata chakula cha mchana.
Sauti ya 2 ya Mratibu wa mradi Bridge Tanzania kitaifa Bi Fatma Shabani Mrope.
Mradi wa Bridge Tanzania umelenga moja kwa moja kuwawezesha Vijana waliotengwa na wanaoishi katika mazingira magumu katika jamii kupata Stadi za Maisha zitakazowawezesha Kuboresha hali zao za kiuchumi