Mufindi FM

Mufindi FM yashika namba 3 kwa kulipa kodi

21 February 2025, 07:10

Mwandishi wa habari wa Mufindi Jumane Bulali, akiwa ameshikilia tuzo ya mlipa Kodi mkoa wa Iringa, kwa niaba ya Meneja Mufindi FM.

na Jumane Bulali

Mufindi FM Radio 107.3 imeshika nafasi ya tatu Kwa kulipa Kodi Kwa wakati na kwa usahihi Kwa upande wa Vyombo vya Habari vya Mkoa wa Iringa.

Mufindi FM imepewa tunzo hiyo maalumu baada ya kutambuliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Iringa wakati wa usiku wa Utolewaji wa Tuzo kwa walipa Kodi wa nyaja mbalimbali.

Akizungumza wakati wa Utolewaji wa Tuzo hizo Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh. Peter Serukamba mbali na kuwapongeza Washindi mbalimbali pia ametoa wito Kwa Wafanyabiashara kulipa Kodi kwa hiyari.