Micheweni FM

RC Kaskazini Pemba afanya ziara ya kushtukiza shehia ya Utaani kukagua usafi wa mazingira

17 September 2026, 12:45 pm

Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya akiwa kwenye ziaza ya kukagua usafi wa mazingira katika shehia ya Utaani wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba (picha na Mwiaba Kombo)

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mhe Mgeni Khatib Yahya, amefanya ziara ya kushtukiza katika Shehia ya Utaani, ambapo amekagua hali ya usafi wa mazingira na kuwataka wananchi kuongeza juhudi katika kuhifadhi usafi wa maeneo yao ili kuepuka milipuko ya magonjwa na kujenga mazingira salama na yenye afya kwa jamii.

Na Mwiaba Kombo

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amesisitiza kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi, huku akiwataka viongozi wa Shehia kushirikiana na wananchi kuhakikisha taka zinakusanywa na maeneo ya makazi yanakuwa safi wakati wote.

sauti ya mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya

Kwa upande wao Mkuu wa Wilaya ya Wete, Abdalla Rashid Ali, pamoja na Mkurugenzi wa Baraza la Mji Wete, Shuwena Hamad Ali, wamewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika usafi wa mazingira, wakisisitiza kuwa usafi si jukumu la Serikali pekee bali ni wajibu wa kila mwananchi.

Sauti ya mkuu wa Wilaya ya Wete, Abdalla Rashid Ali, pamoja na Mkurugenzi wa Baraza la Mji Wete, Shuwena Hamad Ali

Nao baadhi ya wananchi wameahidi kudumisha usafi wa mazingira huku wakitoa wito kwa wananchi kushirikiana kuweka mazingira katika hali ya ya usalama.

Sauti ya Mohammed Foum..Mkazi wa Shehia ya Utaani
Mwajuma Ramadhan Hassan…..Mkazi wa shehia ya Utaani.