Micheweni FM

Viongozi wa dini Micheweni watakiwa kusimamia watoto kupata elimu

17 September 2026, 1:25 pm

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya akizungumza na wazazi ,walezi ,walimu ,wanafunzi pamoja na viongozi mbali mbali katika mdahalo ulioandaliwa na kituo cha Redio Jamii Micheweni huko skuli ya Karume Shumba Mjini(Picha na Shaaban Ali)

Wananchi  wa  Wilaya ya Micheweni wamesema wamekuwa sehemu ya mafanikio ya elimu ya watoto wao kwa kufuatilia kwa karibu maendeleo yao  kielimu , wakisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kuhakikisha watoto wanafanya vizuri na kufikia malengo yao ya kielimu.

Na Masanja Mabula.

Wakizungumza katika mdahalo maalum ulioandaliwa na kituo cha redio Jamii Micheweni chini ya ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, huko Shumba ya Mjini wananchi hao wamesema wamekuwa wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya watoto wao skuli , pamoja na kushirikiana na walimu katika kutatua changamoto zinazoweza kuathiri masomo yao.

Nao baadhi ya viongozi walioshiriki mdahalo huo, akiwemo Afisa Elimu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba pamoja na mwakilishi wa UNESCO, wamewataka wanafunzi kuwa tayari kukabiliana na changamoto zinazoweza kukwamisha maendeleo yao kielimu, huku wakisisitiza umuhimu wa kujituma katika masomo na kutumia fursa zinazopatikana.

Sauti ya Ismaili Ali Hamad ….Afisa Elimu Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Ali Masoud Kombo….Meneja wa Redio jamii Michheweni
Hasina Bukhti….Msimamizi wa Mradi UNESCO

Akifungua mdahalo huo, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mgeni Khatib Yahya, amewataka viongozi wa dini kutumia nafasi na ushawishi walionao kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu, hususan kwa watoto na vijana.

Sauti ya Mgeni Khatib Yahya…..Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Mdahalo huo umeweka msisitizo juu ya umuhimu wa ushirikiano wa wadau wote wa elimu katika kuhakikisha watoto wanapata elimu bora na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zinazoweza kuathiri maendeleo yao kielimu.