Micheweni FM
Micheweni FM
7 July 2025, 7:42 pm

Chama cha wananchi CUF ni miongoni mwa chama cha siasa ambacho kitashiriki uchaguzi mkuu Taifa ambao unatarajiwa kufanyika October 2025 ambapo viongozi wa chama hicho wamewataka wanachama wao pamoja na wananchi kwa ujumla kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kwenye uchaguzi huo kwa kupiga kura ili kuweza kuwachagua viongozi ambao ni bora na watakao ongoza majimbo na taifa kwa ujumla .
Na Mwiaba Kombo
Chama cha wananchi CUF Taifa kimewata kawatia nia katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kufahamu kuwa watakapopata ridhaa ya kugombea nafasi hizo kuwa wapo kwa ajili ya kuwatumikiawananchi.
Kauli hiyo imetolewa na katibu mkuu wa chama hicho Taifa Husna Mohd Abdalla wakati alipokuwa akizungumza na Viongozi wa chama hicho ngazi ya Matawi , majimbo na Wilaya huko katika ukumbi wa Samail Gombani Pemba amesema mwanasiasa yeyote ambae atagombea nafasi na kubahatika kuchaguliwa ajue kwamba amepata nafasi hio kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na sio chama chake.
Akizungumzia kuhusu wanawake amesema chama chake kitahakikisha kinawapa fursa wanawake nahawapati changamoto yoyote katika mchakato wa kugombania nafasi za uongozi.
Kwa upandewake NaibuMkurugenzi wa habari kutoka chama cha CUF Ali Rashid Abarani amewataka wachama ambao niwajumbe watakaoshiriki katika kuwapigia kura watiania kuwa niwajumbe kutoka tawi husika ili atakaechaguliwa awe ni kutoka jimbo lililokusudiwa
Nae Mjumbe wa baraza kuu taifaHasina Mohammed Sharif amewataka wanawake kujitokeza kuchukuafomu za kugombania nafasi mbalimbali za uongozi bila ya woga kwani wanachama wote wanahakisawa katika chama .
Mapema viongozi hao pamoja na wanachama wa chama hicho wamezindua tawi jipya machomanne Chake chake Pemba.