Savvy FM

Zaidi ya mataifa 23 duniani yakutana kujadili usawa wa kijinsia Arusha

3 March 2026, 2:09 pm

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima akizungumza na waandishi wa habari. Picha na Mariam Mallya

Mkutano wa kimataifa wa mafunzo ya usawa na jinsia, ulemavu na ujumuishwaji wa kijamii umezikutanisha nchi zaidi ya 23 duniani lengo likiwa ni kujadili namna yakuendelea kuhudumia jamii kwa kuzingatia usawa wa kijinsia kwa makundi yenye mahitaji maalumu.

Na Mariam Mallya

Mara baada ya kufungua mkutano huo uliofanyika jijini Arusha, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalumu Dorothy Gwajima amesema dhumuni kubwa ni kujadili maswala ya usawa wa kijinsia kwa watu wenye ulemavu kwani mazingira yanapaswa kuwekwa vizuri kwa ajili yao ili waweze kufikia malengo yao.

Sauti ya Waziri wa maendeleo, jamii, njisia, wanawake na makundi maalumu, Dorothy Gwajima

Naye Mkurugenzi mkuu wa shirika la World vision Tanzania, James Anditi ameeleza umuhimu wa jukwaa hilo na kusema kuwa taifa haliwezi kusonga mbele kama halitowapatia watu wenye mahitaji maalum vipaumbele.

Sauti ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la World vision Tanzania, James Anditi

Jukwaa hilo la kimataifa linabebwa na kauli mbiu isemayo “Kubadili Mitazamo, Kuvunja Vikwazo na Kufungua Fursa,” hii ikitajwa kuchochea usawa wa kijinsia katika jamii kwa kuzingatia makundi yote muhimu kuanzia ngazi ya familia.