Savvy FM
Savvy FM
3 Machi 2026, 23:13

Wananchi wa jiji la Arusha wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yatakayofanyika kimkoa siku ya Machi 05/2026 katika viwanja vya Ngarenaro mkoani Arusha.
Na Mariam Mallya
Akizungumza katika Studio za Savvy FM Mratibu wa jinsia halmashauri ya jiji la Arusha Angelina Christian amesema mkoa huo umejipanga vizuri kuhakikisha maadhimisho hayo yanafanyika vizuri nakuwataka wajasiriamali kuleta bidhaa zao ili kujitangaza.
Aidha Mratibu wa jinsia halmashauri ya jiji la Arusha Angelina Christian amewasihi wanaume kujitokeza katika maadhimisho ya siku ya wanawake na kusema hakuna maendeleo ya mwanamke bila mwanaume.
Naye Afisa maendeleo Habiba Madebe amesema maswala ya kijinsia na maendeleo ya mwanamke hayawezi kusonga mbele bila kupata ushirikiano kutoka kwa wanaume.