Savvy FM

Wafugaji waonywa matumizi ya ARV kwa mifugo

April 23, 2025, 1:56 pm

Picha na maktaba/dawa za ARV na mifugo

Kuelekea kilele cha siku ya maadhimisho ya kitaifa ya utoaji wa huduma za afya ya wanyama ambayo itafanyika April 26 mwaka huu,wadau  na  wafugaji wametakiwa kuacha tabia za kutumia dawa za ARV ili kunenepesha mifugo

Na Mzidalifa Saidi.

Akizungumza leo  Daktari mkuu wa wanyama kutoka Halmashauri ya mji wa Babati  Dkt Fatuma Mkombozi amesema kwa mkoa wa Manyara bado hawajapata kesi inayohusiana na matumizi ya ARV kwa mifugo na kusema wafugaji wa mijini wanapaswa kufuga michache ili iwe na tija.

Sauti ya Dkt Fatuma Mkombozi

Aidha,maadhimisho hayo ni ya tatu tangu kuanza  na mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu inayosema “Mafanikio ya afya ya wanyama yanahitaji ushirikiano “

.