Micheweni FM

Pemba wamuunga mkono Rais Dkt. Mwinyi

5 September 2025, 11:09 am

Mwananchi wa kijiji cha Maziwang’ombe Khatib Mjanawe Arafa akizungumza na wahariri na waandishi mbali mbali kutoka Tanzania bara na Zanzibar picha na (Mwiaba Kombo)

Wananchi kisiwani Pemba wamesema hawajawahi kushuhudia maendeleo makubwa kama yale yaliyopatikana ndani ya kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Na Mwiaba Kombo

Wakizungumza na wahariri na waandishi wa habari kutoka Tanzania Bara na Zanzibar waliotembelea miradi mbalimbali kisiwani humo, wananchi hao wamesema utekelezaji wa miradi hiyo ni kielelezo cha utekelezaji mzuri wa ahadi za serikali.

Khatib Mjanawe Arafa, mkazi wa kijiji cha Maziwang’ombe, amesema wananchi wa kijiji hicho wanajivunia hatua za maendeleo zilizofikiwa na wameahidi kumpa kura nyingi Dkt. Mwinyi katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu.

sauti mwananchi Khatib Mjanawe kutoka kijiji cha Maziwang’ombe Micheweni

Naye Alawia Hamadi Ali, pia kutoka kijiji hicho, amesema wananchi walikuwa na hamu kubwa ya kuona maendeleo, na kwamba ujio wa Dkt. Mwinyi umewezesha miradi mingi muhimu kutekelezwa katika kijiji chao.

Wananchi hao wamesema wako tayari kumuona Dkt. Mwinyi akiendelea kuiongoza Zanzibar kwa miaka mingi zaidi, wakisisitiza kuwa ndiye chaguo sahihi kwao.

sauti ya Alawia Hamad Ali kutoka kijiji cha Maziwang’ombe