Ileje FM

Shilingi bilioni 1.9 wakopeshwa vijana Tunduma

June 18, 2025, 1:17 pm

Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Mohamed Kawainda akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mjiji Tunduma.Picha na Denis Sinkonde

Vijana wametakiwa kuchangamkia fursa ya asilimia ya mikopo inayotolewa na hamashauri mji Tunduma kwa lengo la kuinua uchumi wao.

Na:Denis Sinkonde

Halmashauri ya Mji wa Tunduma wilaya ya Momba Mkoani Songwe kwa kipindi cha uongozi wa serikali ya Awamu ya sita imetoa kiasi cha zaidi ya Bilioni 1.9 kwa vijana ikiwa ni mikopo ya asilimia 10% kutoka mapato ya ndani.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Momba Elias Mwandombo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Tunduma mbele ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohamed  kawaida amesema kuwa wananchi wa mkoa wa Songwe wanampongeza na kumshukuru Rais Samia kwa fedha nyingi alizozitoa kwaajili ya maendeleo ya mkoa huo zikiwemo fedha kwaajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalumu.

sauti mkuu wa wilaya ya Momba

Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe Ladiwil Mwampashi amemuomba Kawaida kufikisha kilio cha Barabara ya njia nne katika mji wa Tunduma ili kuweza kurahisisha shughuli za usafishaji na biashara.

SAuti ya mwenyekiti CCM mkoa wa Songwe

Akiongea na wananchi wa Tunduma Mkoani Songwe kwenye mkutano wa huo Mwenyekiti wa Uvccm Taifa Mohamed Kawaida amesema uchaguzi hapa nchini ni kama kifo hauepukiki na kuongeza kuwa chama chake tayari kimejiandaa kunadi ilani yake ili kupata ridhaa ya Watanzania.

Kawaida ameongeza kuwa chama cha Mapinduzi kinajiamini kuelekea kwenye uchaguzi kwasababu kinayo mambo mengi ya kuwaeleza wananchi huku mengine wakiwa wanayaona wenyewe.

sauti mwenyekiti Uvccm Taifa
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohammed Ali Kawaida akikagua Ukarabati unaoendelea katika Hospitali ya Mkoa wa Songwe.Picha na Denis Sinkonde