Ileje FM

Wananchi wachimba mashimo na kujisaidia kwa kukosa vyoo

May 10, 2024, 2:49 pm

Hii ni moja ya choo kinachotumiwa na moja ya familia katika kijiji cha Mkutano wilayani Momba mkaoni Songwe{picha na Denis Sinkonde}

Na Denis Sinkonde, Songwe

Jumla ya kaya 128 kati ya 320 katka Kijiji cha Mkutano Wilaya ya Momba mkoani Songwe hazina vyoo, huku kaya 34 pekee ndizo zenye vyoo bora sawa na asilimia 17.

Hayo yamebainishwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dkt. Boniface Kasululu mara baada ya kufanya zoezi la ukaguzi wa vyoo bora kwa kupita nyumba kwa nyumba kijijini hapo.

Dkt Kasululu amewapongeza wenyeviti wa vitongoji kwa kuzitambua kaya ambazo hazina vyoo ambapo wamezibaini kaya ambazo hazina vyoo.

Aidha Dkt Kasululu amesema wananchi hawa wanachimba mashimo vichakani kwa ajili ya kujisaidia na kufukia kila siku kwa kukosa vyoo.

“Katika ukaguzi huu hatujabahatika kukuta vinyesi vichakani bali tumekuta wananchi wanajisaidia vichakani kwa kuchima mashimo,”amesema Dkt. Kasululu

Sauti ya mganga mkuu mkoa wa Songwe Dkt. Boniface Ksululu

Julias Sanane mwenyekiti wa kijiji hicho amekiri kijiji kaya nyingi kukosa vyoo hali ambayo inaweza sababisha mlipuko wa magonjwa  kutokana na ukosefu wa vyoo bora.

Sauti ya mwenyekiti wa kijiji Julias Sanane

Nao baadhi ya viongozi wa dini ambao walihudhuria ukaguzi wa vyoo kwenyekijiji hicho wamesema.

Sauti za viongozi wa dini………………….