Aridhi
Ruangwa FM

Wanawake Lindi wataka elimu zaidi umiliki wa ardhi

14 September 2026, 12:02

Eneo la ardhi ya kijiji Cha Namkatila.picha na Omari Mdigo.

Wanawake waomba elimu zaidi juu ya Umiliki Ardhi kisheria huku mfumo dume ukitajwa kua kikwazo

Na Omari Mdigo.

Ruangwa – Lindi.

Baadhi ya wanawake Mkoa wa Lindi wameeleza kuwa umiliki wa ardhi umewapa usalama wa mali na fursa za kiuchumi, huku wakitaka elimu zaidi kuhusu haki zao za kisheria.

Mayasa Joroa amesema changamoto si mila pekee, bali pia ukosefu wa uelewa kuhusu taratibu na haki za wanawake katika umiliki wa ardhi.

sauti za wanawake

Takwimu zinaonesha Mkoa wa Lindi, asilimia 18 ya wanawake wenye miaka 15 na zaidi wanamiliki ardhi peke yao, ikilinganishwa na asilimia 22.7 ya wanaume.

Aidha, zaidi ya hati 7,300 za ardhi zimesajiliwa Lindi, huku wanawake wakiwa na hati 832 pekee za umiliki binafsi, sawa na asilimia 11.4.

Msajili wa hati mkoa wa Lindi Massua.

Wadau wanasisitiza kuwa mwanamke ana haki ya kumiliki, kusajili, kutumia na kunufaika na ardhi bila kubaguliwa kwa misingi ya jinsia.

Ardhi si mali ya mwanaume pekee elimu, usajili na uelewa wa haki ni msingi wa kuongeza usalama wa umiliki kwa wanawake.