Ruangwa FM
Ruangwa FM
23 June 2026, 14:14

Wananchi wengi Ruangwa watajwa kununua maeneo kiholela jambo ambalo limesababisha migogoro ya Aridhi na kuwakosesha haki za kisheria za umiliki wa Aridhi.
Akizungumza 22 June Afisa Maendeleo ya Aridhi Isihaka Panja amesema migogoro mingi imefika ofisini hapo huku baadhi yao ni wananchi kuvamia maeneo ya kijamii, migogoro ya mipaka na kuingia katika maeneo ya hifadhi.
Akizungumzia upatikanaji wa Aridhi Tanzania mwanasheria wa Halimashauri ya wilaya ya Ruangwa Levina Ado amesema ikiwa umegaiwa , umerithi,upewa,ama kununua Aridhi bila ya kufuata taratibu za aridhi utakua mkaaji Haramu wa Aridhi
Nao Viongozi wa serikali ya kijiji wamewataka wananchi kutoishia ofisi za vijiji pekee kwani Maridhiano ya hati ya kijiji hayampi jamii uhalali kamili wa umiliki wa eneo husika.

Hata hivyo Baadhi ya wananchi wamezungumzia uelewa wao katika umiliki wa Aridhi huku wakitaja kukosa haki kwani wengi huuziana Kiundugu.