Triple A FM

Kwa Mrombo kupata soko la kisasa

13 January 2026, 10:59 am

Mkuu wa mkoa wa Arusha mh. Amos Makalla (katikati) akikagua ramani ya soko jipya linalojengwa kwa Mrombo

Na Joel Headman

Wananchi wa kwa Mrombo jiji la Arusha wanatarajia kunufaika na ujenzi wa soko jipya la kwa Morombo ambalo tayari ujenzi wake umeanza.

Wafanyabiashara hao wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 500 waliokuwa wakifanya biashara eneo hilo awali hawakuwa na soko la kisasa ambapo ujenzi wa sasa ukikamilika unatarajiwa kuwa na wafanyabiashara zaidi ya 700

Akikagua maendeleo ya ujenzi wa soko hilo mkuu wa mkoa wa Arusha Amos amewataka wakandarasi wanaotekeleza mradi huo kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kwa viwango

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Arusha mh. Amos Makala

Pia mkuu wa mkoa ameurai uongozi wa jiji la Arusha kuhakikisha wafanyabiashara wa awali wanapewa kipaumbele katika ugawaji wa maeneo ya biashara (vizimba) kwenye soko hilo INS..Makala

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Arusha mh. Amos Makala