Triple A FM

Fountain Gate waanza na Mungu

17 October 2025, 7:46 pm

Wachezaji wa Fountain Gate wakipambania mpira

Na Joel Headman

Ndivyo unavyoweza kusema baada ya ushindi wa bao 1 la dakika za jioni walilolipata Fountain Gate dhidi ya Dodoma jiji jioni ya leo

Mchezo huo wa ligi kuu uliopigwa kwenye dimba la Tanzanite Kwaraa umeshuhudia kandanda safi lililotembezwa na timu zote mbili huku kukiwa na mashambulizi ya kupokezana

Kabla ya mchezo huu wa leo Fountain gate walikuwa na kauli mbiu inayosema “Tunaanza na Mungu” n ahata wakati wachezaji wakiingia uwanjani kwa Pamoja na Mashabiki na raisi wat imu hiyo walionekana kusimama na kuimba wimbo wa The Mafik Tunaanza na Mungu mpaka walipokanyaga pictch kisha mashabiki na rais wakapiga makofi na kukaa

Ni kama mchezo ulikua unamalizika bila ya goli kwa pande zote mbili kwani mpaka dakika ya 90 ilikua bila bila na kunako dakika ya 2 kati ya zilizoongezwa ndipo Mudrik Shehe alimalizia krosi safi iliyopigwa kutoka Magharibi mwa uwanja na Jimyson mwinuke na kuiandikia Fountain goli pekee la ushindi

Baada ya mchezo kocha wa Fountain Gate Mohamed Laizer amewashukuru wachezaji na mashabiki kwa namna walivyojitoa na kujipatia ushindi

Kocha wa Fountain Gate Mohamed Laizer

Kwa upande wa kocha wa Dodoma Jiji Amani Josia amesifu uwezo wachezaji wake licha ya kupoteza na kusema ni sehemu ya mchezo na kuwa watafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza INS….Josia

Kocha wa Dodoma Jiji Amani Josia