Triple A FM

Mkude “Changamkieni fursa AFCON”

24 September 2025, 3:04 pm

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude akizungumza na waandishi wa habari (Picha na ofisi ya mkuu wa Wilaya)

Na Daudi Peter

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude amewataka wananchi kuwa tayari na kujiandaa kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazoletwa na mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kufanyika mwaka 2027

Akizungumza na Triple A Mkude amesema kuwa michuano hiyo imefungua fursa kwa wananchi kujiongezea kipato kwani kutakuwa na muingiliano mkubwa wa watu na hivyo wajiandae kutoa huduma zinazoendana na hadhi ya mashindano hayo

Akizungumza kwa upande wa maandalizi ya uwanja ameeleza kuwa mpaka sasa ni zaidi ya 60% na kwamba mradi huo utakamilika kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude akizungumza na waandishi wa habari