Triple A FM

UDP kuifanya Arusha kitovu cha utalii wa michezo

24 September 2025, 2:35 pm

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha United Democratic Party (UDP) bi.Saum Rashid akihutubia wananchi kwenye kituo kikuu cha mabasi Arusha. Picha na Joel Headman

“Suala zima la riadha,suala zima la mpira wa miguu,mpira wa mikono,mpira wa pete na michezo aina nyinginezo nyingi kwa sababu tunaona fursa ya ajira”

Na Joel Headman

Mgombeau rais wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha United Democratic Party (UDP) bi.Saum Rashid ameahidi kuinua pato la mkoa wa Arusha kupitia utalii wa michezo

Akijibu swali la mwandishi wa Triple A aliloulizwa kwenye mkutano wa kampeni alioufanya jana kituo kikuu cha mabasi Arusha, Bi Saum amesema atashughulikia suala hilo kwa haraka mara tu atakapochaguliwa kuwa raisi.

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha United Democratic Party (UDP) bi.Saum Rashid akihutubia wananchi kwenye kituo kikuu cha mabasi Arusha.

Kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na ukwepaji wa kodi ameahidi kushughulikia suala hilo ikiwemo kuweka mifumo mizuri ambayo haitamuumiza mfanyabiashara na  itakuwa inamvutia kulipa kodi kwa hiari

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha United Democratic Party (UDP) bi.Saum Rashid akihutubia wananchi kwenye kituo kikuu cha mabasi Arusha.