Triple A FM

Kocha Singida alivyowamudu Simba, bado Yanga

31 May 2025, 6:53 pm

Mchezaji wa Singida Black Stars Emmanuel Keyeke (kulia) akishangilia baada ya kuifungia timu yake goli

Na Joel Headman Babati

Ushindi wa 3-1 dhidi ya Simba ni kama umewapa mzuka sana Singida United aisee

Mnyama Simba sasa hana lake tena kwenye mashindano ya shirikisho Tanzania kwani kwa kipigo hicho wameaga rasmi mashindano hayo

Mechi hii ni kama ya kulipa kisasi kwa Simba baada ya kupata ushindi wa 1-0 Dar Es Salaam ushindi ambao ulilalamikiwa

Akizungumza Kocha wa Singida BS David Ouma amesema si mara ya kwanza Kuifunga Simba na kuwa ataendelea kuwafunga vigogo wa soka nchini

Kocha wa Singida BS David Ouma

Kwa upande wa Fadlu Davis wa Simba ameshukuru wachezaji kwa uwezo wa kujitoa na kuwa hawezi kulalamikia ratiba ya michezo ambayo hata hivyo sio rafiki

Kocha wa Simba Fadlu Davis