Triple A FM

Mchungaji kutekwa Arusha mapya yaibuka

18 May 2025, 6:00 pm

Mchungaji Steven Jacob Katika ibada ya ubatizo mwezi Machi 2025

Na Joel Headman

Saa chache baada ya kupatikana kwa mchungaji wa kanisa la huduma ya Kristo lililopo Kata ya Muriet mtaa wa FFU mkoani Arusha Steven Jacob, mapya yameibuka leo kanisani kwake

Ibada ya leo Jumapili iliyofanyika kanisani hapo, imeshuhudiwa ikiongozwa na mchungaji Vulfrida George badala ya mchungaji Steven.

Katika mahubiri hayo mchungaji Vulfrida ameeleza kuwa bado wana Imani kubwa kwa Mungu kuwa anaweza kufanya mambo yanayoonekana hayawezekani.

Ameeleza kuwa kanisa linaendelea kufanya maombi kwani ndio yanaweza kuwashindia katika hali wanayopitia

Sauti ya mchungaji Vulfrida George katika mahubiri yake leo

Mchungaji Steven Jacob anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana Ijumaa ya wiki hii mei 16 kabla ya baadaye kupatikana wilayani Siha mkoani Kilimajaro.

Hata hivyo baada ya kupatikana siku ya Jumamosi Mei 17 amezungumza na waandishi wa habari na kuelezea yaliyomkuta.

Sauti ya mchungaji Steven Jacob akielezea tukio lililomtokea

Wakati akielezea kupotea kwa mwanae, baba mzazi wa mchungaji huyo Jacob Gumbo ambaye pia ni balozi wa nyumba 10 kwenye eneo hilo amekemea matendo maovu yanayofanywa kwa watumishi

Sauti ya Jacob Gumbo baba mzazi wa mchungaji Steven

Bado tunaendelea kutafuta jeshi la polisi mkoani hapa kuhusu uthibitisho wa tukio hili na kinachoendelea mpaka sasa