Micheweni FM

Kilio cha muda mrefu kwa shule za shumba vyamboni na Tumbe chatatuliwa

18 July 2025, 10:48 am

Mbunge wa jimbo la Tumbe Amour Khamis Mbarouk akizungumza na walimu ,kamati za shule pamoja wanafunzi waliofika kwa ajili ya kushuhudia makabidhino ya mashine za fotokopi (picha na Mwiaba Kombo)

Shule za shumba vyamboni masingi Tumbe na Tumbe Sekondari ni miongoni mwa shule ambazo zilikuwa na kilio cha muda mrefu wa kupata huduma ya fotokopi kwa ajili ya kutolea mitihani ya wanafuni pamoja na shughuli nyengine za kiofisi ,kilio hicho kimepata ufumbuzi baada ya mbunge wao wa jimbo hilo kuweza kuwapelekea mashine hizo ambazo zitatumika kwa matumizi ya ofisi.

Na Mwiaba Kombo

WALIMU wa skuli za shumba vyambo msingi ,tumbe msingi na Sekondari wametakiwa kuzitumia mashine za fotokopi ambazo wamepewa kwa lengo la kurahisisha kazi zao ili wanafunzi wapate kuafaulu vizuri .

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mbunge wa jimbo la Tumbe Amour Khamis Mbarouk amewataka walimu kuhakikisha kwamba lengo la fotokopi hizo zinatumika kama ambavyo imekusudiwa

Kwa upande wake mwenyekiti wa skuli ya shumba vyamboni  msingi  Salim Khamis Abdalla  wameahidi kuvitunza vifaa hivo na kuvitumia kama ambao imekusudiwa kwani kilikuwa ni kilio cha muda mrefu kwao.

Wakitoa neon la shukrani mwalimu mkuu skuli ya Tumbe Sekondari Asha Rashid Abdalla pamoja na mwalimu mkuu skuli ya shumba vyamboni msingi Seif Khamis Ali  wamempongeza mbunge mstaafu huyo kwa kuweza kuwatatulia kilio cha muda mrefu ambacho kilikuwa kikiwakabili katika skuli zao.