Triple A FM

Arusha ipo tayari

28 October 2025, 10:55 am

Mkuu wa mkoa wa Arusha CPA Amos Makalla

“nimekutana na Kamati zote za usalama wilaya ndani ya Mkoa na tumejiridhisha kuwa kampeni zimeenda salama kwa amani na utulivu katika Majimbo yote na hali ya usalama katika Wilaya zote ni shwari.”

Na Furahini Jonas

Mkuu wa mkoa wa Arusha mh.Amos Makala amewahakikishai wananchi usalama kabla wakati na baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika kesho Oct 29-2025

Makala amewasisitiza wananchi kudumisha amani na utulivu katika zoezi zima la uchaguzi na pia kujitokeza kushiriki zoezi hilo

Mkuu wa mkoa wa Arusha CPA Amos Mkalla

Kwa upande mwingine mkuu wa Wilaya ya Arusha mjini Joseph Mkude amethibitisha kuwa vifaa vyote vinavyohitajika kwa ajili ya uchaguzi kwenye wilaya hiyo vimeshapokelewa na vipo tayari kwa matumizi ndani ya mitaa 154 na vituo 1051 vitakavyotumika kupigia kura

Mkuu wa wilaya ya Arusha Joseph Mkude

Wananchi wa mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla wenye sifa watashiriki zoezi la uchaguzi ambapo watapata fursa ya kuwachagua madiwani, Wabunge na rais kwa mujibu wa katiba ya nchi