Triple A FM

Hatma ya Ngorongoro baada ya uchaguzi

3 September 2025, 10:48 am

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla (Picha na ofisi ya mkuu wa mkoa)

Na Joel Headman

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla amewataka wananchi wa Wilaya ya Ngorngoro kuwa watulivu na kuendelea kudumisha amani na Mshikamano wakati wakisubiri majibu ya Tume mbili zilizoundwa kushughulikia changamoto zao.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Sale Kata ya Sale wilayani Ngorongoro amebainisha kuwa tayari ripoti ya tume mbili zilizoundwa na raisi zimeshakabisdhiwa na zitatolewa maamuzi baada ya uchaguzi mkuu wa 2025

Sauri ya mkuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla

Amewaomba viongozi wa kimila wa eneo la Ngorongoro kusaidia kudumisha hali ya Amani.

Sauti ya kuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla

Rais Samia wakati alipokutana na Viongozi wa Jamii ya Kimasai Mkoani Arusha alitangaza kuunda tume mbili, Moja ikihusika na tathmini kuhusu masuala ya ardhi yanayolalamikiwa na wakazi wa eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na ya pili ilipewa kazi ya kuangalia utekelezaji wa uhamaji wa hiari kutoka eneo la hifadhi kwenda Msomera, Wilayani Handeni Mkoani Tanga