Uvinza FM

Elimu yatolewa kwa vikundi vya wajasiriamali wa wilaya ya Uvinza

15 May 2025, 8:31 pm

Vikundi tofauti vya wananchi vikipata mafunzo ya asilimia kumi ya mkopo wa halmashauri wilayani Uvinza katika ukumbi wa ofisi ya kata ya Uvinza(Picha na Linda Dismas)

Vikundi vya wajasiriamali wa halamashauri ya wilaya ya Uvinza waanza kunufaika na elimu iliyoanza kutolewa hii leo mei 15 juu ya mkopo wa asilimia kumi wa mama Samia.

Na Linda Dismas

Vikundi vya ujasiriamali katika wilaya ya Uvinza leo Mei 15, 2025 wameanza mafunzo ya ujasiriamali yatakao chukua muda wa siku sita, kwa lengo la kupewa elimu kabla ya kupatiwa fedha ya mikopo ya asilimia 10 itakayo wasaidia kujikwamua kiuchumi.

Picha ya maafisa maendeleo ya jamii wilaya ya uvinza, kulia ni Bi. Leah Stanilei Mjema.

Akizungumza na uvinza fm redio Bi.Leah Stanilei Mjema ambaye ni afisa maendeleo ya jamii wilaya ya Uvinza amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha mwanakikundi anakuwa na uelewa mkubwa wa namna ya kukuza biashara zao mara tuu wanapopata mkopo.

Sauti ya Afisa Maendeleo ya jamii Bi.Leah Stanilei Mjema 1

 Aidha amewataka akina baba kuonyesha ushirikiano wao kwa kina mama waliochukua mkopo wa asilimia 10 ili kufikia malengo yao ya kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya Afisa Maendeleo ya jamii Bi.Leah Stanilei Mjema 2

Vilele Bi.Leah amewashauri wananchi kutumia fursa hiyo ya mkopo wa Mama Samia ili kuendeleza shughuli zao za kibiashara na ujasiriamali.

Sauti ya Afisa Maendeleo ya jamii Bi.Leah Stanilei Mjema 3
Afisa Mtendaji kata ya Uvinza Bw. Edward Amos.

Naye mtendaji wa kata ya Uvinza Bw.Edward Amos amesema ni vyema kila mwanakikundi kutambua katiba ya kikundi inasemaje ili kuepusha migogoro.

Sauti ya mtendaji wa kata ya Uvinza Bw.Edwad Amos 1

Akijibu swali liloulizwa na mmoja wa wanavikundi hivyo vya ujasiriamali “ni kwanini baadhi ya fomu za mikopo zinaenda kwenye kikundi zikiwa na muhuri wa mtendaji ila jina sio lake” ambapo mtendaji amejibu kuwa kila mtu atambue kuwa cheo sio mtu wala jina la mtu.

Sauti ya mtendaji wa kata ya Uvinza Bw.Edward Amos 2

Nae Fadhila Sadick mmoja wa kikundi cha RAHA DELICIOUS ametoa shukrani zake kwa viongozi wa maendeleo ya jamii kwa kuwapa elimu ya namna ya kuendesha biashara pale tuu watakapopata mikopo ili iweze kuwasaidia kukuza biashara zao.