Uvinza FM

Wazazi wapeni watoto elimu ya kijinsia bila kupepesa macho

12 May 2025, 2:36 pm

Wanafunzi wa shule ya msingi muungano walioshiriki katika kipindi cha watoto cha shool baraza.Picha na Theresia Damasi

Toka kuundwe kwa dawati la kijinsia katika shule hiyo wanafunzi wamepata elimu ya kufahamu  madhara ya mimba za utotoni na kufahamu namna ya kuepuka vishawishi

Na Theresia Damasi

Katika kuhakikisha ukatili dhidi ya watoto unakomeshwa na kupingwa vikali katika jamii,Shule ya msingi muungano katika halmashauri ya wilaya uvinza imeeunda dawati la ukatili kwa ajili ya kuwapa watoto elimu ya njinsi ya kukabiliana nao.

Wakizungumza na uvinza fm redio katika kipindi cha school Baraza wanafunzi wa darasa la sita na la saba wamesema toka kuundwe kwa dawati la kijinsia katika shule hiyo wamepata elimu ya kufahamu  madhara ya mimba za utotoni na kufahamu namna ya kuepuka vishawishi.

Sauti za wanafunzi wakieleza madhara ya mimba za utotoni 1

Katika kupanua mjadala wa mada ya madhara ya mimba za utotoni wanafunzi hao wameeleza ni wapi wanapaswa kutoa taarifa wanapofanyiwa ukatili.

Sauti za wanafunzi wakieleza maeneo ya kutoa taarifa 2
mmoja ya mwanafunzi akichangia mada katika kipindi cha watoto cha shool baraza

Naye mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi muungano Paulo Mandai ameeleza umuhimu wa dawati la jinsia katika shule hiyo ambapo amesema wazazi wawape watoto elimu ya kijinsia bila kupepesa macho.

Sauti ya Mwalimu 1

Hata hivyo mwalimu Mandai ameeleza chanzo cha mimba za utotoni huku akiwataka wazazi wawe walimu wa kwanza kuwafundisha watoto maadili mema na kupinga ukatili unaofanywa dhidi ya watoto.

Sauti ya mwalimu