Uvinza FM

Bima ya afya kwa wote sasa bure kwa kaya masikini

3 February 2026, 1:21 am

Madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya kusulu wakiwa katika kikao. Picha na Emmanual kamangu

Naomba mkatoe elimu kwa wananchi na kuhakikisha wanaelewa mkakati wa serikali wa kutoa bima ya  afya kwa wote 

Na. Emmanual Kamangu

Wanufaika kaya masikini TASAF  elfu 66800 mkoani kigoma  Kunufaika bure na bima ya afya kwa wote ikiwa ni mpango wa serikali kuendelea kutoa huduma bora za afya  kwa kaya  ambazo hazijiwezi.

Mkuu wa wilaya ya kasulu Kanal Isack Mwakisu akizungumza na madiwani wa halmashauri  ya wilaya ya kasulu amewaomba kutoa elimu kwa wananchi kuhakikisha wanaelewa mkakati wa serikali wa kutoa bima ya  afya kwa wote  zoezi ambalo linategewa kuanza  bure kwa  kaya masikini Tasaf.

Sauti ya 2 Mkuu wa wilaya ya kasulu Kanal Isack Mwakisu
Picha ya Mkuu wa wilaya ya kasulu Kanal Isack Mwakisu. picha na Emmanual Kamangu

Aidha Kanal Mwakisu amesema kuwa baada ya zoezi hilo kukamilika kwa kaya masikini Tasaf litahamia kwa jamii nzima  ambapo wanafamilia sita watanufaika na bima ya afya kwa kiwango cha Tsh  laki moja na elfu hamsini pekee  na kuwasaidia  kupata huduma bure za afya kuanzia ngazi ya zahanati na kuendelea.

Sauti ya 2 Mkuu wa wilaya ya kasulu Kanal Isack Mwakisu

Fabiano Dangi  Doragi ni  diwani wa kata ya rusesa ambaye ni mmoja wa madiwani ambao wameshiriki mkutano huo amepongeza serikali kwa kuja na mpango wa bima ya afya kwa wote jambo litakalosaidia kwa kiasi kikubwa wananchi kupata matibabu  kwa wakati na kuimalisha afya zao.

Sauti ya Fabiano Dangi  Doragi ni  diwani wa kata ya Rusesa