Uvinza FM
Uvinza FM
2 October 2025, 7:11 pm

Wananchi wametakiwa kushilikiana na serikali katika kuibua changamoto ya unyanyasaji wa kijinsia unaofanyika kwa wazee.
Na Dunia Stephano
Kaimu mtendaji ambaye pia ni Afisa maendeleo wa kata ya nguruka wilaya ya Uvinza Sarafina jonijo mapasi amewataka wananchi kushilikiana na serikali katika kuibua changamoto ya unyanyasaji wa kijinsia unaofanyika kwa wazee.
Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wazee katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wazee duniani iliyofanyika nguruka iliyokuwa na kaulimbiu isemayo wazee tushiriki uchaguzi kwa ustawi wa jamii.
Sauti mtendaji kata
Kwa upande wake Afisa ustawi wa jamii kata ya nguruka Miraji pazi ameyataka mashirika ya serikali na yale yasio ya kiserikali kuendelea kushirikiana kwa pamoja kwani ushirikiano ndio nguzo na heshima katika kuleta utu.

Sauti afisa ustawi
Aidha afisa tabibu kutoka kituo cha afya nguruka Ado Crispini mapunda amewataka wazee kuhudhuria kliniki kwa ajiiri ya kuendelea na kupima magonjwa yasiyoyakuambukizwa ikiwemo magonjwa ya moyo na shinikizo la damu.
Sauti afisa tabibu
Kwa upande wao wazee waliohudhuria tukio hilo wamesema kuwa vijana wanapaswa kuwavumilia wazee wao na wawaheshimu kutokana na uzee wao .
Sauti wazee
Ikumbukwe kuwa tukio hilo la siku ya wazee dunia katika kata nguruka limehudhuriwa na watu mbalimbali ambao wamefanikisha shuguli ikiwemo uvinza paralegal foundation,nguruka development agency pamoja na SMAUJATA Uvinza.