Uvinza FM

Mahwa: Jimbo la Kigoma Kusini sio shamba la bibi

1 October 2025, 11:40 am

Mgombea wa ubunge jimbo la Kigoma Kusini  kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMA BW. Eliya Mahwa picha na Glory Paschal.

Nitahakikisha  naishauri serikali kurekebisha sheria na sera rafiki za uwekezaji ili vijana wanaosoma wapate ajira rasmi.” Eliya Mahwa

Na. Theresia Damasi

Mgombea wa ubunge jimbo la Kigoma Kusini  kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMA BW. Eliya Mahwa amesema kuwa atarudisha hadhi na heshima ya elimu endapo atapata ridhaa kwa wananchi  kuongoza jimbo hilo.

Amesema hayo kwenye kipindi cha kumekucha na uvinza fm   kuwa atahakikisha  anaishauri serikali kurekebisha sheria na sera rafiki za uwekezaji ili vijana wanaosoma wapate ajira rasmi huku ambao hawajapata elimu  waweze kujiajiri wenyewe .

sauti ya mgombea wa ubunge jimbo la Kigoma Kusini CHAUMA BW. Eliya Mahwa

Sanjari na hayo Mgombea huyo   amesema kuwa migogoro mingi ya ardhi inatokana na wingi wa watu na mifugo ambapo  michoro ya ardhi imechorwa muda mrefu hivyo kuna umuhimu wa serikali kutambua ongezeko na  uhitaji wa ardhi pamoja na kupitia upya mipaka kwa kurasimisha kutokana na mahitaji ya sasa.

sauti ya mgombea wa ubunge jimbo la Kigoma Kusini CHAUMA BW. Eliya Mahwa

Aidha Mgombea  Mahwa amesema wananchi wa jimbo la Kigoma Kusini wamepata tabu ya kukosa maji safi na salama kwa mda mrefu, ambapo atahakikisha anaenda kuweka miundombinu kwa siku 90 pale  anapochaguliwa kuwa mbunge.

sauti ya mgombea wa ubunge jimbo la Kigoma Kusini CHAUMA BW. Eliya Mahwa

Pamoja na hayo ila ya chama cha ukombozi {CHAUMA}kwa mwaka 2025 hadi 2030 inasema itasimamia Madaraka ya umma,Maadili ya uongozi, Lishe kwa wote, Utawala Bora,Ardhi maendeleo ya watu na Elimu Bora .