Uvinza FM

Vikundi vya wajasiriamali Uvinza vyapatiwa elimu ya msaada wa kisheria

17 May 2025, 12:36 am

Vikundi tofauti tofauti vya wajasiriamali vikipata elimu ya msaada wa kisheria katika ukumbi wa ofisi ya kata ya Uvinza(Picha na Linda Dismas)

Wananchi watumieni maafisa maendeleo jamii dawati la msaada wa kisheria kupata elimu ya kisheria ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima hasa migogoro ya ardhi na mirathi.

Na Linda Dismas

Ikiwa leo ni siku ya pili ya muendelezo wa elimu juu ya mkopo wa asilimia kumi wa Mama Samia, maafisa maendeleo jamii dawati la msaada wa kisheria wilaya ya Uvinza hii leo wamewapatia elimu ya mirathi wajasiriamali hao.

Picha ya afisa maendeleo ya jamii dawati la msaada wa kisheria Bi.Janeth Mwakibete.

Akizungumza na Uvinza fm radio Bi.Janeth Mwakibete amesema kuwa wanashirikiana na jeshi la polisi katika kutoa elimu ya msaada wa kisheria kwa wananchi wasio kuwa na elimu hiyo na hata wale ambao wanayo lakini bado wamepoteza haki zao za msingi.

Sauti ya Bi.Janeth Mwakibete 1

Bi.Janeth ameendelea kwa kusema dawati la msaada wa kisheria limekuwa likihakikisha wanaifikia jamii kila mara ili kutambua changamoto zinazowakumba.

Sauti ya Bi.Janeth Mwakibete 2

Aidha ameeleza kuwa wamekuwa wakipokea kesi za mara kwa mara zinazotokana na ukatili wa kijinsia hususani kwa kina mama na watoto na hivyo kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuripoti matukio hayo ili kupata msaada wa kisheria wa haki zao.

Sauti ya Bi.Janeth Mwakibete 3

Nao baadhi ya wajasiriamali katika mafunzo hayo wameeleza namna walivyonufaika na elimu hiyo ya mirathi na kuwasihi wananchi wengine wawe na mazoea ya kujitokeza katika mafunzo mbalimbali yanayotolewa na serikali ili kuwasaidia kutambua haki zao za msingi.

Sauti za wanavikundi vya ujasiriamali

Hata hivyo ikumbukwe kuwa lengo la elimu ya mirathi ni kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake ya msingi.