ADHANA FM DIGITAL

CCM Kaskazini Unguja yashauriwa kutatua changamoto za wakulima

7 July 2024, 7:06 am

Na Juma Haji Adhana FM.

Mbunge Wa Jimbo La Chaani Juma Usonge ameishauri Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa waskazini Unguja kutatua changamoto za wakulima wa bonde la mpunga Kibokwa ili kufikia lengo la serikali kupitia sekta ya Kilimo hapa nchini.

Ameyasema hayo katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM mkoa wa Kaskazini Unguja kilichofanyika Mahonda katika Ofisi za chama hicho  kwa lengo  la kusikiliza utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imefanywa na serikali.

Aidha amewashauri viongozi wanaosimamia Sekta ya kilimo  kufanya utafiti wa  mabondea ya kilimo ili kufahamu aina ya kilimo kinachotakiwa kulimwa katika maeneo hayo jambo ambalo litakalosadia kuleta mapinduzi ya kilimo kwa wakulima.