Uvinza FM

Waziri Mavunde azindua chumvi lishe ya mifugo Nyanza Uvinza

15 August 2025, 6:57 pm

Waziri wa madini Athony Mavunde pamoja na watumishi wengine wa serikali wakikagua chumvi inayodhalishwa katika kiwanda cha nyanza salt uvinza

Waziri mavunde amesema Kiwanda cha Nyanza kina msaada mkubwa katika kuchangia pato la taifa na kuzindua chumvi lishe ya wanyama ni mwanzo mzuri wa maendeleo nchini.

Na Theresia Damasi

Waziri wa madini Anthony Mavunde amezindua bidhaa mpya ya chumvi lishe ya mifugo {cattle Lick} katika kiwanda cha chumvi nyanza salt katika wilaya ya uvinza mkoani Kigoma ambapo bidhaa hiyo itakuwa inasaidia mifugo kuwa na afya nzuri na virutubisho,ambapo hapo awali wafanyabiashara nchini Tanzania walikuwa wanaagiza kutoka nje ya nchi.

Waziri Mavunde akihutubia wananchi na wadau baada ya kukagua mashamba ya chumvi nyanza

Akizindua bidhaa hiyo Waziri mavunde amesema Kiwanda cha Nyanza kina msaada mkubwa katika kuchangia pato la taifa na kuzindua chumvi lishe ya mifugo ni mwanzo mzuri wa maendeleo nchini na kwa mkoa mzima wa kigoma.

Sauti ya Waziri wa madini Athony Mavunde

Waziri Mavunde amesema amefarijika kuzindua bidhaa ya cattle Lick ya mifugo hivyo anawaomba wafanyabiashara kuwaunga mkono nyanza salt kwa kazi kubwa ambayo wanayoifanya na kuacha kuagiza bidhaa hiyo nje ya nchi kwani tayari bidhaa inapatikana nchini.

Sauti ya Waziri wa madini Athony Mavunde

Kwa upande wake Dinnah Mathamani  Mkuu wa wilaya ya uvinza  amesema kiwanda cha nyanza salt kina mchango mkubwa wa kupandisha uchumi katika wilaya ya uvinza kwani kimezalisha ajira kwa asilimia kubwa na kwa upande wa masoko kinaongeza ufanisi wa ndani na nje.

Mkuu wa wilaya ya uvinza Dinnah Mathaman akiambatana na Waziri Mavunde pamoja na wamiliki wa kiwanda cha chumvi wakifanya ukaguzi katika mashamba ya chumvi uvinza

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya uvinza Dinnah Mathaman

Kadhalika mkurugenzi mkuu wa halmashauri ya uvinza Fred Milanzi amesema bidhaa ya cattle lick katika halmashauri yake ni fursa kwani wafugaji ni wengi huku ufugaji ukiendelea kukua ambapo anamatumaini bidhaa hiyo inaenda kuwa mkombozi kwa wafugaji wote ambapo mifugo inaenda kuwa na afya.

Sauti ya Mkurugenzi wa halmashauri ya uvinza Fredi Milanzi

Nao baadhi ya wananchi na wafanyakazi waajiriwa katika  kiwanda cha Nyanza salt wameeleza manufaa wanayoyapata hasa kujipatia riziki kwa njia ya ajira waliyonayo katika kiwanda hicho ambapo kupitia fursa hiyo familia zinapata mahitaji yote na kujikwamua kiuchumi.

Picha ni wafanyakazi na wadau wakiwa katika uzinduzi wa bidhaa mpya ya lishe ya mifugo katika kiwanda cha chumvi

Hata hivyo kiwanda cha Nyanza salt kipo wilaya uvinza katika mkoa wa kigoma kimetoa ajira kwa wazawa wa mkoa wa kigoma na ambao sio wazawa kwa asilimia kubwa pia kinachangia  pato la taifa kwa ukubwa wenye maendeleo endelevu.