Tumbatu FM

Ukosefu wa elimu ya ndoa chanzo cha migogoro ya familia

11 January 2026, 11:23 am

Picha ya walimu wa madrsa na maimamu wa misikiti wakiwa katika mafunzo kuhusu elimu ya ndoa yanayotolewa na jumuiya ya Nataraji Social Devlopment Foundation (NSDF) ya Kisiwani Tumbatu(Picha na Vuai Juma)

“Kukosekana kwa taaluma kabla ya kuingia kwenye ndoa hasa kwa vijana wa sasa hupelekea migogoro na kuongezeka kwa wimbi la talaka”

Na Vuai Juma

Viongozi wa dini wametakiwa kuwahimiza wanajamii   kujifunza elimu ya ndoa ili kujiepusha  na migogoro ndani  ya familia.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa jumuiya ya Nataraji Social Devlopment Foundation Sidik Juma Khamis wakati akizungumza na maimamu pamoja na walimu wa madrasa katika mwendelezo wa mafunzo ya elimu ya ndoa yaliyofanyika katika tawi la skuli ya Vivid Dream Tumbatu Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema lengo kubwa la kuwapa elimu viongozi hao ni kuitengeneza jamii katika mfumo mzima wa maisha ya ndoa kwani kumekuwa na matatizo mengi ambayo yanawakumba wanandoa kwa kuikosa elimu hiyo.

Ni sauti ya mwenyekiti wa jumuiya ya Nataraji Social Devlopment Foundation Sidik Juma Khamis.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo  ukhut Namboto Khamis Juma amesema ipo haja ya kuendelea kutolewa mafunzo hayo kwa vijana  kutokana matatizo yaliyomo kwenye ndoa ambayo yanasababishwa na mporomoko wa maadili.

Sauti ya mshiriki wa mafunzo  Ukhut Namboto Khamis Juma akizungumza kwa niaba ya washiriki wezake.