Tumbatu FM

Jiandikisheni mapema kwa ajili ya ibada ya Hijja

3 August 2025, 2:34 pm

Ni waumini wa dini ya kiislam kisiwani Tumbatu wakiwa katika hafla ya utowaji wa elimu kuhusu maandalizi ya ibada ya hija (Picha na Juma Haji.

“Tuwahutubie waumini wa dini ya kiislam kuhusu hijja kumekuwa na mabadiliko kwa wale wanaotaka kwenda Makka wanatakiwa kujiandikisha mapema huu ni utaratibu uliowekwa na uongozi wa Makaa”

Na Juma Haji Juma

Mashekh na maimamu Nchini wametakiwa kutoa khotba ya kuelimisha umma juu ya umuhimu wa kujisajili mapema kwa wananchi wenye nia ya kushiriki ibada ya hija mwaka 1447 hijria.

Akielezea utaratibu wa ibada ya hijja ya mwaka 2025 sawa na mwaka 1447 hijiria kwa wananchi wa Tumbatu katika hafla ya kutoa Elimu juu ya umuhimu ya kuhifadhi historia ya kiislam Mkurugenzi wa Wakfu Amana na Hijja kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana  Hajjat, Madina Haji Khamis amesema  utaratibu uliozoweleka wa kutoa hotba za hija kwenye miskiti katika mwezi wa ramadhani hautosaidia kufikisha elimu kwa wakati.

Hajjat, Madina amesema kuwa kutokana na ongezeko la watu wenye uhitaji ya ibada ya hijja Nchi ya makka imeweka ukomo wa kupokea majina ya mahujjaji mwezi 20 shaaban kwa hija ya mwaka huu na yoyote atakaejitokeza kuomba nafasi ya kuhiji atapangiwa  mwaka unaofuata.

Sauti ya mkurugenzi wa Wakfu Amana na Hijja kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana  Hajjat, Madina Haji Khamis.

Aidha amesema katika kuhakikisha kila mwananchi anapata uwezo wa kuhiji Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Zanzibar imeazisha mfuko wa hijja ambao  utamuwezesha mwananchi mwenye kipato cha chini kuweka akiba kwa ajili ya mataarisho ya safari ya hijja.

Ni sauti No.2 ya mkurugenzi wa Wakfu Amana na Hijja kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana  Hajjat, Madina Haji Khamis.

Akizungumzia swala la kuweka wakfu wa mali Shekh Mohamed Ali Mohamed kutoka Kamisheni ya Wakfu amesema ili kuepusha waislamu kuwa omba omba  ni lazima watu wenye uwezo kuweka mali zao wakfu ili zisaidie uendeshaji wa shughuli za uislamu.

Aidha Shekh Mohamed amewataka waislam wa sasa kuwaiga wasilam waliopita ambao waliekeza nguvu na mali zao kusaidia  huduma za miskiti, madrasa na kutoa misaada kwa mayatima na watu wasiojiweza.

Sauti ya Shekh Mohamed Ali Mohamed kutoka Kamisheni ya Wakfu.

Wakitoa shukuran baadhi ya washiriki wa hafla hiyo Mw Juma Omar Juma, Mw Jecha Ali Saleh na wananchi wa Tumbatu kwa ujumla wameishukuru Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana  kuwapatia elimu na kuwataka kuendeleza utamaduni huo wa kutembelea waislam.

Ni sauti za walimu wa madrasa Tumbatu Jongowe.

Ziara ya hiyo ilihusu kuhamasisha wananchi kuhifadhi nyaraka Pamoja na Mejngo  ya historia ya kisiwani Tumbatu sambamba na   kutembelea mjengo ya historia yaliyopo eneo la Makutani pamoja na kutoa Sadaka ya  misahafu, Chaki Pamoja na  Nguo kwa watoto wa Tumbatu.