Tumbatu FM

Tunzeni rasilimali za bahari kuongeza kipato

1 July 2025, 11:04 am

Picha ya viongozi wa jumuiya ya Jongoe Development Foundation wakiwa kwenye kipindi Radio jamii Tumbatu (picha na Vuai Juma)

“Ili kufikia dhamira ya uchumi wa bluu lazima tutunze mazingira kwenye bahari kwa kuepuka kuharibu mazalia ya Samaki”

Na Vuai Juma

Wananchi wametakiwa kulinda  na kutunza rasilimali za bahari ili kuendeleza dhana ya uchumi wa buluu kama ilivyo azma ya serikali ya kuajiri watu wengi ndani ya sekta ya uvuvi.

Kauli hiyo imetolewa na  Ndugu  Ali Makame  kutoka idara ya maendeleo ya uvuvi na mazao ya baharini   wakati akizungumza na wakazi wa mkoa wa kaskazini unguja kwenye kipindi maalum kuhusu sualazima la utunzaji wa mazingira  ambacho kimerushwa kupitia kituo  cha radio jamii Tumbatu.

Amesema ili jamii iweze kupata maendeleo  kupitia kazi ya uvuvi ni lazima kuwe na utaratibu wa kuhifadhi mazingira katika maeneo ya Bahari.

Sautu ya 1 ndugu Ali Makame kutoka idara ya maendeleo ya uvuvi na mazao ya baharini.  

Hata hivyo amesema serikali imekuwa ikishirikiana na wadau mbali mbali katika kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira Baharini lakini bado kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya watu kutofika maeneo ya kutoa elimu hiyo jambo ambalo linasababisha kuongezeka kwa uharibifu wa rasilimali za Bahari huku akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi wakati wa kutolewa kwa taaluma inayohusu masuala ya Bahari.

Sautu ya 2 ndugu Ali Makame.

Kwaupande wake Shehe Awesu  Shehe Afisa miradi wa jumuiya ya Jongowe  Developmenti  Foundation  amesema sekta ya uvuvi inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi  na uvuvi haramu mambo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kuathiri mazingira na viumbe wa baharini.

Sauti ya Afisa miradi wa jumuiya ya Jongowe  Development  Foundation  Shehe Awesu  Shehe.