Tumbatu FM

Viongozi watakiwa kutoa taarifa kwa wananchi

1 July 2025, 10:00 am

Pichani ni mkuu wa Mkoa Kaskazini Unguja Matar Zahoro Masoud akiwa na wandishi wa habari kwenye kikao ofisini kwake Mkokotoni. (Picha na Vuai Juma)

“Viongozi wote wanawajibu wa kutoa taari ili wananchi waweze kuzifaham na kujua kinacho endelea”

Na Vuai Juma.

Watendaji wa sekta za kiserikali ndani ya mkoa wa Kaskazini Unguja wametakiwa kutoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu utendaji wao ili kuweza kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wananchi.

Akizungumza  na wandishi wa Habari huko ofisini kwake Mkokotoni  Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja  Matar Zahoro Masoud  amesema viongozi wote wanawajibu wa kueleza tarifa kwa wandishi wa Habari ili waweze kuwafikishia wananchi walio chini  hasa maeneo ya vijijini.

Amesema  tayari amekwisha toa maagizo kwa  wakuu waote wa taasisi zilizo chini yake kuhakikisha wanatoa tarifafa ambazo wanajamii wanapaswa kuzifaham  hali itakayopelekea kutanua wigo wa mawasiliano kati ya serikali na watu wake.

Sauti nambari 1 ya Mkuu wa Mkoa Kaskazini Unguja Matar zahoro Masoud.

Hata hivyo amewataka wandishi wa Habari kujiepusha na utowaji  taarifa ambazo zitaleta taharuki katika jamii ili taifa liweze kubaki salama na kupiga hatua kubwa za kimaendeleo.

Sauti nambari 2 ya Mkuu wa Mkoa Kaskazini Unguja Matar zahoro Masoud.