Kahama FM
Kahama FM
March 25, 2026, 4:25 pm

Na Sebastian Mnakaya
Watoto takribani 145,820 wanatarajiwa kufikiwa na chanjo ya polio Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga huku watoa huduma ya chanjo wakitarajia kuwafikia watoto hao nyumba kwa nyumba, stend, sokoni, shule, vituo vya kulea watoto na kliniki.
Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa Kahama Dkt. Herry Sylivester amesema hayo leo kwenye uzinduzi wa utoaji wa chanjo huku akieleza watoto wanao takiwa kupata chanjo ni wenye umri chini ya miaka kumi.

Dkt. Sylivester amesema uhamasishaji umefanyika kwa njia mbalimbali ili kuweza kuwafikia walengwa kupata chango ya polio, huku akisema mtoto asipopata chanjo hiyo na akipata ugonjwa wa polio unaweza kumsababishia ulemavu wa kudumu wakati mwingine kifo.

Kwa upande wao, baadhi ya wazazi ambayo watoto wao wamepatiwa chanjo hiyo akiwemo Rehema Mngaya na Christina Lucas wameishukuru serikali kwa kutoa chanjo hiyo ambayo itawasaidia watoto wao wasipate magonjwa wa polio.
Vimelea vya ugonjwa wa polio vimebainika mkoani Mwanza kwenye majitaka na hivyo serikali kuchukua jukumu la utoaji wa chanjo kwa mikoa saba ya Kanda ya Ziwa ikiwa hapa nchini Tanzania mgonjwa wa polio mara ya mwisho alibainika mwaka 1996.