Kahama FM

Kahama yatakiwa kuwapa motisha wauguzi

May 31, 2025, 3:34 pm

Mkuu wa wilaya ya Kahama akiwa katikati wa wauguzi wa halmashauri ya Manispaa ya Kahama (picha na Sebastian Mnakaya)

Waaguzi katika Manispaa ya Kahama wamepewe motisha kutokana na kazi ngumu na hatarishi wanayofanya

Na Sebastian Mnakaya

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita amemuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya kahama Masudi Kibetu kutoa motisha kwa wauguzi wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi ikiwemo kuwahudumia wenye magonjwa ya kuambukiza.

Mboni ameyasema hayo leo wakati akizungumza katika mahadhimisho ya siku ya wauguzi duniani ambapo kwa wilaya ya Kahama yamefanyika katika kituo cha afya Nyasubi kilichopo Manispaa ya Kahama, .

sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita

Aidha, Mhita ameiomba halmashauri ya Manispaa ya Kahama kutenga bajeti kwa ajili ya wauguzi hao kupata mafunzo mbali mbalimbali yanayohusu taaluma yao, ikiwemo mikutano na makongamano, huku Manispaa hiyo ikitakiwa kuendelea kutekeleza miradi ya ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na nyumba za watumishi.

sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita

Awali akisoma risala ya Katibu wa Chama cha Wauguzi Manispaa ya Kahama Agnes Mkanga amesema kuwa wauguzi hawapewi motisha ya mazingira hatarishi licha ya kuwahudumia wagonjwa wa kifua kikuu,homa ya ini na magonjwa mengine ya kuambukiza.

Katibu wa Chama cha Wauguzi Manispaa ya Kahama Agnes Mkanga

Siku ya wauguzi duniani huadhimishwa kila ifikapo May 12 ya kila mwaka, Na kwa mwaka 2025 kauli mbiu ni “Uuguzi Nguvu ya Mabadiliko”

Katibu wa Chama cha Wauguzi Manispaa ya Kahama Agnes Mkanga akisoma risala mbele ya mkuu wa wilaya ya Kahama