Vwawa FM Radio

Muziki wawaongezea utulivu Ng’ombe wakati wa kukamuliwa

November 20, 2025, 3:02 pm

Ng’ombe akiwa amewekewa muziki pembeni maanadalizi ya kukamuliwa. Picha na Anyisile Fredy

Asajile amekuwa akiwasoma Ng’ombe wake tabia hii humsaidia kupata maziwa kwa wingi zaidi

Na Anyisile Fredy

MKAZI na mfugaji wa ng’ombe  wa maziwa mjini Vwawa Mbozi Mkoani Songwe, Mikaya Asajile amesema  amewagundua  ng’ombe wake kwamba wanapenda muziki wakati wa kukamuliwa.

Amesema hayo alipozungumza na Vwawa Fm iliyoshuhudia muziki kwenye zizi wakati Asajile akiwakamua ng’ombe hao.

Sauti ya Mikaya Asajile 1

Mfugaji huyo ambaye ni kijana asiyependa uzururaji  bali kazi za kilimo na ufugaji amesema awali alikuwa akiwapa pumba ng’ombe wake wakati wa kuwakamua, lakini sasa anatumia muziki.

Sauti ya Mikaya Asajile 2

Asajile ambaye ana mke na watoto na mcheshi  wa tabia amesema amekuwa akiwasoma ng’ombe wake tabia kwani wanatofautinana. Amesema aliloligundua kwa ng’ombe wake ni kupenda burudani.

Ametaja aina ya muziki wanaopenda n’gombe wake.

Sauti ya Mikaya Asajile 3