Vwawa FM Radio

Wenye watoto chini ya miaka 5 wakumbushwa umuhimu wa kliniki

6 June 2025, 12:39 pm

Baadhi ya wanawake waliofika kwenye kliniki Isangu Mbozi mkoani Songwe.Picha na Mpiga picha wetu

Ni pamoja na kupata elimu ya lishe bora na afya ya watoto

Na Mwandishi wetu

Wazazi na walezi wa watoto chini ya miaka mitano kitongoji cha Isangu Mbozi mkoani Songwe  wamehimizwa kufika kliniki na kuwalisha watoto chakula bora ili wakue wakiwa na afya ya mwili na akili.

Mtoa huduma ya afya ngazi ya jamii  wa kitongoji hicho , Mary Mwashilindi alisema hayo alipotoa elimu ya jinsi ya kulisha watoto kwenye kliniki ya kupima kila mwezi ambayo wazazi wanakutana kituo cha godauni kupima watoto badala ya kwenda Hospitali ya Vwawa ambako ni mbali.

Mary aliwasihi wanaonyonyesha kuendelea  kuwanyonyesha watoto wao huku wakizingatia masuala ya kuwalisha vyakula vya aina mbalimbali yakiwamo matunda.

Sauti ya Mary Mwashilindi

Aidha Diwani wa Kata ya Hasanga Mbozi Mh.Malick Nzowa aliwapongeza wazazi waliofika kwa wingi kwenye kliniki hiyo na kwamba inafanyika hapo  kwa muda na kwamba malengo ya baadaye ni huduma zote zifanyike kwenye kituo cha afya ambacho kinaendelea kujengwa Isangu.

Alitoa wito kwa wenye watoto kufika kwenye kliniki kujua maendeleo yao.

Sauti ya diwani wa Kata ya Hasanga Mbozi Mh.Malick Nzowa

Aidha baadhi ya wanawake wameeleza  mambo wanayopata kwenye kliniki hiyo. Wanawake wengine wakiwa na watoto wao wametaja yaliyojiri kwenye kliniki  ya jana.

Sauti za wanawake waliohudhuria kliniki