Vwawa FM Radio

Wananchi Isangu walalamikia ubovu wa barabara

April 23, 2025, 12:53 pm

Hali halisi ya barabara ya Isangu kwenda Iyela. Picha na Kennedy Sichone

Ubovu wa barabara wakwamisha wananchi kutofanya shughuli za maendeleo

Na Kennedy Sichone

HASANGA

Wananchi wa kitongoji cha Isangu kata ya Hasanga wilayani Mbozi mkoani Songwe wamelalamikia ubovu wa barabara ya kutoka Isangu kwenda kitongoji cha Iyela. Wakizungumza na Vwawa FM Radio, wananchi hao wamesema barabara hiyo imekuwa ni kikwazo kikubwa kwa shughuli zao za kila siku, hasa upande wa usafiri wa abiria na mizigo.

Mkazi wa Kata ya Hasanga Lydia

Wananchi wamesema hali mbaya ya barabara hiyo inasababisha vyombo vya usafiri kama pikipiki na magari kuharibika mara kwa mara, hivyo kuongeza gharama za matengenezo kwa wamiliki wa vyombo hivyo. Aidha, wameeleza kuwa wakati wa mvua, barabara hiyo huwa haipitiki kabisa, jambo linalosababisha wananchi kushindwa kufikia huduma muhimu kama masoko, vituo vya afya na shule.

Sauti za wananchi

Akifafanua kuhusu kero hiyo, diwani wa kata ya Hasanga, Mheshimiwa Malick Nzowa, amesema tayari wamepokea fedha kutoka mfuko wa jimbo la Vwawa kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya ukarabati wa barabara hiyo. Diwani amesema hatua za awali za maandalizi ya ukarabati huo zimeanza na wanatarajia kazi hiyo itaanza mara moja baada ya taratibu kukamilika.

Sauti ya Diwani Mh.Malick Nzowa akizungumzia ukarabati wa barabara