

24 February 2025, 11:11 pm
Wanafunzi wamepata mafunzo ya namna ya urushaji wa matangazo redioni, ikiwa wapo katika kujifunza mada ya Antena.
Na Theresia Damas
Wanafunzi katika shule ya msingi Nyambutwe wilayani uvinza wamepata mafunzo ya namna ya urushaji wa matangazo redioni, ikiwa wapo katika kujifunza mada ya Antena katika somo la sayansi.
Wakizungumza mara baada ya mafunzo wanafunzi hao wamesema wamepata maarifa maakubwa baada ya kujifunza kwa vitendo huku wakiwaomba walimu kutenga mda wa kutembelea maeneo ili kujifunza kwa vitendo Zaidi.
Sauti ya wanafunzi.
Kwa upande wake Jane Ndalichako mwalimu mkuu wa shule hiyo amesema amefurahishwa na kitendo cha wanafunzi wake kupata mafuzo kwa vitendo kwani yatawasaidia Zaidi katika kumbukumbu zao na kujiongezea maarifa.
Sauti ya Mwalimu Ndalichako.
Ameendelea na kusema kuwa wakazi wa wilaya ya uvinza na viunga vyake watumie fursa ya kutangaza biashara zao na kueleza changamoto zinazowasibu kupitia redio jamii uvinza fm.
Sauti ya Mwalimu Ndalichako.
Naye mwalimu Salehi Hamisi Mteka ameishukuru redio uvinza fm kwa kuweka vipindi vya watoto ambavyo vinatoa elimu mbalimbali ikiwemo masuala ya ukatili huku akiwaomba wazazi kuwaruhusu watoto wao kuhudhuria vipindi pale wanapohitajika kujifunza.
Sauti ya Mwalimu Salehi Mteka.