Uvinza FM

Hakikisheni mnafahamu vituo vya kupigia kura

20 October 2025, 6:54 pm

Picha ya Msimamizi wa uchaguzi jimbo la kasulu vijijini bwana Emmanuel Ladslaus, picha na Emmanuel kamangu

wananchi  mfike kwenye vituo vya kupiga kura ili kutambua mapema kama majina yenu yapo kwenye orodha

Na Emmanuel kamangu

Wananchi wilayani kasulu wamearifiwa kuhakikisha wanafahamu  kwa wakati  vituo watakavyopigia kura  kabla ya siku yenyewe ya octoba 29  ambayo ni siku ya kuwachagua madiwani , wabunge na Raisi.

Akizungumza na wandishi wa habari msimamizi wa uchaguzi jimbo la kasulu vijijini Bw, Emmanuel Ladslausi amesema vituo vya uchaguzi vitafunguliwa saa moja  asubuhi na kufunga saa kumi jioni ili kutoa fursa kwa  wananchi waliowengi kupiga kura.

Sauti ya Msimamizi wa uchaguzi jimbo la kasulu vijijini bwana Emmanuel Ladslaus

Aidha Bw, Ladslausi amewataka wananchi  kufika katika vituo vyao vya kupiga kura ili kutambua mapema kama majina yao yapo kwenye orodha ya kuwachagua madiwani, Wabunge na Raisi.

Sauti ya Msimamizi wa uchaguzi jimbo la kasulu vijijini bwana Emmanuel Ladslaus

Hata hivyo Bw, Ladslaus amesema kwa  wananchi   ambao wamepoteza vitambulisho vya mpiga kura wataruhusiwa kuchagua endapo watakuwa na Lesen ya udereva au kitambulisho cha Nida.

Sauti ya Msimamizi wa uchaguzi jimbo la kasulu vijijini bwana Emmanuel Ladslaus

Jimbo la uchaguzi la kasulu  vijijini linajumula ya vyama sita vya siasa  ambavyo vinashiriki uchaguzi huu wa octoba 29,huku kila chama kikiendelea kunadi sera zake ili kupata ridhha ya kuwaongoza wananchi.