Uvinza FM

Wananchi watakiwa kuiamini tume huru ya uchaguzi Uvinza

2 October 2025, 3:55 pm

Upande wa kushoto ni Msimamizi wa uchaguzi kata ya Uvinza Amos Nkanga akimkabidhi mfano wa fomu ya kupiga kura mgombea udiwani ACT wazalendo Himidi Kisobwe Himidi.

Hili ni zoezi la utoaji wa fomu za mfano za kuweka tiki kwa mgombea atakaye chaguliwa, ili iwe rahisi kutumika katika mikutano ya ugombea udiwani wakati wa kunadi sera zao.

Na Dunia Stephano

Msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni mtendaji kata ya Uvinza Edward Amosi Nkanga  amewataka  wananchi kuwa na imani na tume huru ya uchaguzi wakati wa kupiga kura ukifika na waachane na kauli ya kulinda kura kwani ni kiashiria cha uvunjifu wa amani.

Amesema hayo ofisini kwake alipokuwa akifanya mazungumzo na uvinza fm wakati wa utoaji wa form za mfano za kuweka tiki kwa mgombea watakao mchagua ili iwe rahisi kutumika katika mikutano ya ugombea udiwani wa kata hiyo kutumia kuonesha watakavyo piga kura .

Sauti msimamizi wa uchaguzi kata

Aidha  mgombea udiwani kupitia tiketi ya chama cha Act wazalendo ameahidi kuwa atawaunganisha wananchi wa Uvinza kuwa kitu kimoja bila kujali itikadi ya vyama, dini wala kabila .

Sauti Himidi kisobwe

Kwa upande wake mgombea udiwani kupitia tiket ya chama cha mapinduzi CCM Nilis Ntabaye amewahakikishia wananchi wa Uvinza maendeleo pindi atakapopewa ridhaa ya kuwa diwani wa kata ya hiyo.

Picha ni mgombea udiwani wa chama cha mapinduzi Nilis Noah Ntabaye akizungumza na Uvinza fm baada ya kupokea mfano wa fomu ya kupiga kura.

Sauti nilisi noel ntabaye

Ikumbukwe kuwa zoezi hilo ya kukabidhiwa fomu za mfano kwa wagombea zimetolewa na tume huru ya uchaguzi kwa malengo ya wagombea vyama vya siasa kutumia kama sehemu ya kuwaonesha wafuasi wao namna ya kupiga kura .