Uvinza FM

Wanaume watakiwa kusimama imara kulifanya kanisa kuwa na umoja

14 June 2025, 10:24 am

Picha ya wanaume wa kanisa katoliki parokia ya mrubona UWAKA. picha na Emmanuel Kamangu

Kanisa linahitaji wanaume wa kutosha na  wenye moyo thabiti  wa kulitunza kanisa la Mungu.

Na Emmanuel Kamangu

Wanaume wa kanisa katoliki parokia ya mrubona jimbo  katoliki la kigoma wametakiwa kuwa kielelezo cha kanisa ikiwemo kusimama imara katika kulifanya kanisa kuwa na umoja.

Amesema hayo paroko wa parokia ya Mrubona Kasulu mjini Padre Gaspa Balkumutwe katika misa takatifu ambayo imeambatana na sherehe za utume wa wanaume wa katolki Uwaka  parokiani apo ambapo ameleleza kuwa kanisa linahitaji wanaume wa kutosha na  wenye moyo thabiti  wa kulitunza kanisa la Mungu .

sauti ya paroko wa parokia ya Mrubona kasulu mjini Padre Gaspa Balkumutwe

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wanaume wa katoliki Uwaka Parokia ya Mrubona Bw Camilius Tomas amesema wanapokutana wanaume wakatoliki na kufanya hafla mbali mbali ni moja ya kuendelea kujenga  umoja  ikiwemo  kutiana moyo katika kuendelea kushiriki matendo ya huruma kwa kuwatunza wahitaji wenye shida mbali mbali.

sauti ya mwenyekiti wa wanaume wa katoliki Uwaka Parokia ya Mrubona Bw Camilius Tomas

Nao baadhi ya wanaume wakatoliki ambao wameshiriki katika kutaniko hilo wamesema wamepokuwa na sherehe za mara kwa mara za uwaka huwasaidia kukua kiimani pamoja kuwavuta  wanaume wengi zaidi kuingia katika utume huo. Hata hivyo wanaume hao wakatoliki wameongeza kuwa wanawajibu wa kuchochea maendeleo ya kanisa .

sauti za baadhi ya wanaume wakatoliki ambao wameshiriki katika kutaniko hilo.