Uvinza Fm

Siku ya wanawake duniani jamii yaaswa kujitokeza kuiadhimisha

24/02/2022, 4:36 pm

Na,Rosemary Bundala

Kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika tarehe nane mwezi wa tatu kila mwaka jamii imeaswa kujitokeza katika kuadhimisha maadhimisho hayo

Hayo yamezungumzwa na afisa maendeleo ya jamii kutoka wilaya ya uvinza Mkoani Kigoma bi MASTIDIYA NDYETABULA wakati akizungunmza na redio uvinza fm katika kipindi cha Amka na Uvinza fm ambapo ameitaka jamii kubadirika  na kufuata utaratibu ili  kuleta usawa wa maendeleo endelevu katika jamii

Sauti ya afisa maendeleo

Aidha  afisa huyo wa maendeleo  amewata kinababa  pamoja na vijana kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo kwani siku hii haiwalengi kina mama peke yao

Sauti ya afisa maendeleo uvinza

Katika hatua nyingine  bi MASTIDYA  amewataka wanawake kuitumia siku hii kama siku ya kuacha kufanya matendo maovu , ili waweze kudumisha mahusiano yenye usawa

Sauti ya afisa maendeleo

Maadhimisho Siku ya wanawake duniani ilianza kutokana na jitihada za wanawake 15000 mwaka 1908 walio  andamana mjini newyork Marekani , wakidai kupunguziwa muda wa kufanya kazi , kulipwa ujira mdogo na haki ya kupiga  kura na ikumbukwe kauli mbiu ya siku hii ya wana wake duniani kwa mwakaa huu 2022 ni Kizazi cha haki na usawa kwa maendeleo endelevu.