Tumbatu FM

Wazazi toeni ushirikiano katika kuwasimamia wanafunzi

11 August 2025, 9:46 am

Picha ya Mwalimu Mkuu wa skuli ya sekondari Mkokotoni Haji Abdallah Seif ( Picha na Wache Nyange) 

“Ikwa tutashirikiana kwa pamoja katika kuwasimamia watoto wetu tutaweza kuongeza idadi ya ufaulu ndani ya Skuli yetu”

Na Atka Mosi.

Mwalim  Mkuu wa skuli ya sekondari Mkokotoni Haji Abdallah Seif  amewataka wazazi na walezi  kutoa mashirikiano kwa kuwasimamia watoto kupata haki yao ya elimu ili kuongeza idadi kubwa ya ufaulu.

Akizungumza na Tumbatu Fm huko ofisini kwake  Mkokotoni amesema kujengwa kwa skuli hiyo kutasaidia ongezeko la ufaulu kwa wanafuzi na kuondokana na changamoto ya kufuata elimu masafa ya mbali jambo ambalo lilikua linawapa ugumu wazazi kuwapeleka watoto wao katika skuli za mbali.

Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeboresha miundombinu mbali mbali ikiwemo  ya elimu kwa wananchi wake ili kuongeza wataalamu katika nchi huku akitoa wito kwa serikal kuwatatulia changamoto inayowakabili ya kukosa walimu wa masomola sayansi.

Ni sauti ya Mwalimu Mkuu wa skuli ya sekondari Mkokotoni Haji Abdallah Seif

Kwa upandewao wazazi wa wanafunzi wanaosoma skulini hapo wamesema wanajivunia maendeleo yaliyofanywa rais wa Zanzibar dkt  Hussein Ali  Mwinyi  ikiwemo kuwajengea skuli ya gorofa iliopo karibu na maeneo yao hali ambayo imewapa faraja huku wakisema kujengwa kwa skuli hiyo maeneo ya karibu kutawaepusha watoto kufanyiwa vitendo viovu ikiwemo udhalilishaji.

Sauti za wazazi wa wanafunzi wa Skuli ya Mkokotoni
Picha ya wanafunzi wa Skuli ya Sekondari Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja (Picha na Wache Nyange)

“Tunakabiliwa na changamoto nyingi sisi wanafunzi ikiwemo uhaba wa vifaa vya kujifundishia hasa masomo ya sayansi, uhaba wa walimu wa masomo hayo lakini pia hatuna sehemu ya kulala wanafunzi tunajikuta tunalala kwenye vyumba vya madarasa hali ambayo siyo salama kwetu tunaiomba serikali yetu ambayo ni sikivu kututatulia changamoto hizi”

Nao wanafunzi wa Skuli ya Sekondari Mkokotoni wamesema wamefarijika na uwepo wa skuli hiyo mpya ya gorofa na kuahidi kuitunza skuli hiyo huku wakisema wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ambazo zinawarudisha nyuma katika masomo na kuiomba serikali kuwatatulia changamoto hizo zinazowakabili skulini hapo ikiwemo kutokuwepo kwa Dahalia, vifaa vya masomo ya sayani  na uhaba wa walimu ili kuweza kufikia malengo waliyo kusudia.

Ni Sauti za wanafunzi wa Skuli ya Sekondari Mkokotoni.