Tumbatu FM

Uongozi ni fursa kwa wanawake

1 July 2025, 1:43 pm

Picha ya katibu wa umoja wa vijana mkoa kaskazini Unguja Moh’d Ali Moh’d ( Picha na Vuai Juma)

“Wanawake wamekuwa msitari wa mbele kugombania nafasi za uongozi ndani ya mkoa wa kaskazini Unguja hali hii inatuonesha wazi kuwa mkoa wetu umepiga hatua kwenye demokrasia”

Na Vuai Juma

Chama cha mapinduzi mkoa wa Kaskazini Unguja kimesema kinatambua juhudi na michango ya viongozi wanawake katika kuliletea taifa maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na katibu wa umoja wa vijana chama hicho Moh’d Ali Moh’d wakati akizungumza na Radio Jamii Tumbatu huko ofisini kwake mahonda mkoa wa Kasakazini Unguja.

Amesema kwa mwaka huu wanawake wa CCM waliomo kwenye mkoa huo wamehamasika kwa wingi kuchukua fomu za kugombania nafasi za Uongozi kwenye siasa ikiwemo viti maalum kwa vijana  kwa nafasi za uwakilishi ubunge na udiwani  hali inayoonesha namna chama hicho kinavyowaunga mkono wanawake kwenye suala la demokrasia sambamba na kuwataka vijana kushiriki katika uchaguzi mkuu  kwa amani na utulivu.

Sauti ya ndugu Moh’d Ali Moh’d kkatibu wa umoja wa vijana Mkoa Kaskazini Unguja.
Picha ya mbumge viti maalum kwenye nafasi za vijana mkoa kaskazini Unguja Amina Bakari Yussuf (Picha na Vuai Juma)

Kwaupande wake Amina Bakari Yussuf Mbunge viti maalum upande wa vijana mkoa Kaskazini Unguja amesema wanawake waliopata nafasi za kuongoza kwenye ngazi mbali mbali wamekuwa na mchango mkubwa kwenye taifa hili huku akiwataka wanawake vijana na watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi kugombania nafasi za uongozi kwenye ngazi ya siasa  Pamoja na kuendelea  kuungamkono juhudi za serikali.

Ni sauti ya Mbunge viti maalum upande wa vijana mkoa wa kaskazini Unguja Amina Bakari Yussuf.

Zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi  ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) limeanza rasmi tarehe 28 Juni na linatarajiwa kufungwa mnamo tarehe 2 Julai mwaka huu.