Kahama FM

Mabinti wanaoishi mazingira magumu Kahama wafadhiliwa masomo

March 23, 2026, 6:18 pm

Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Swahiba Shemshem akuzungumza na mabinti waliopatiwa ufadhili wa masomo WiLDAF (Picha na Sebastian Mnakaya)

Na Sebastian Mnakaya

Zaidi ya mabinti 18 wanaoishi katika mazingira magumu halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga, wamepatiwa ufadhili na serikali kusomeshwa katika elimu ya ufundi VETA kwa fani mbalimbali, ikiwemo ufundi cherehani na ususi.

Akizungumza wakati wa kuwaaga mabinti hao kuelekea chuoni, Afisa ustawi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Swahiba Shemshem, amesema serikali kwa kushirikia na shirika WiLDAF katika mradi wa Chaguo langu Haki yangu, wameendelea kuwafadhili mabinti hayo, waliokatishwa masomo kutokana na sababu mbalimbali.

Sauti ya Afisa ustawi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Swahiba Shemshem

Aidha, Swhiba amesema kuwa baada ya kumaliza kozi hizo watapatiwa vitendea kazi ili waweze kujiajiri wao wenyewe, huku akiwataka wazazi kuacha tabia ya kuwaozesha watoto wao wakiwa na umri mdogo na badala yake waache wasome ili watimize ndoto zao za baadae.

Sauti ya Afisa ustawi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Swahiba Shemshem
Afisa ustawi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Swahiba Shemshem

Kwa upand wao, baadhi ya mabinti hao wakizungumza kwa nyakati tofauti, akiwemo Hawa Selemani Abduli, Tedy Boniphas na Esther John, wameishukuru serikali kwa kuwapatia ufadhili wa masomo hayo ambayo yatawasaidia katika maisha yao ya baadae.

Sauti za mabinti Hawa Selemani Abduli, Tedy Boniphas na Esther John

Hata hivyo, mpaka sasa zaidi ya mabinti 261waliokatishwa ndoto zao kwa sababu mbalimbali walipatiwa ufadhili huo ambao kila moja kwa sasa anaendelea na shuguli zake.