Kahama FM
Kahama FM
March 20, 2026, 9:18 pm

”Wajasiriamali wa wilaya ya Kahama, changamkieni fursa kupitia jukwaa la Mwanamke Mjasiriamali”
Sebastian Mnakaya
Wanawake wajasiriamali wilayani Kahama mkoani Shinyanga wamezindua jukwaa lao la Mwanamke Mjasiriamali kwa lengo la kusaidiana katika shughuli zao za kujipatia vipato pamoja na mikopo isiyokuwa na masharti magumu.
Kiongozi wa jukwaa hilo Salome Mvanga akizungumza wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo ulifoanyika katika Manispaa ya Kahama, ambapo amesema kuwa lengo la kuwa na jukwaa hilo ni kuwezeshana wanawake kiuchumi na kuinuana katika biashara.

Aidha, Mvanga amesema kuwa wanatarajia kuanzisha tamasha la MWANAMKE MJASILIAMALI ambalo linatarajiwa kufanyika mei mosi mwaka huu 2026, litakalo husisha wajasiliamali mbalimbali wanofanya shughuli zao katika mijini wa Kahama, ikiambana na tuzo mbalimbali.
Mvanga ameongeza kuwa ili wakina mama wajasiliamali wafanikiwe zaidi wanapaswa kushirikiana na kuwa wamoja katika shughuli zao, huku akiwataka kuchangamikia fursa ya kushiriki katika tuzo zinazoandaliwa na Mwanamke Mjasiriamali.

Kwa upande wao, baadhi ya wajasiliamali akimwemo Grace Zagamba na Delmas Mathias, wamesema kuwa jukaa hilo litawasaidia wakina mama kuinua, kuzionesha na kuziendeleza biashara zao pamoja na kupata mikopo nafuu kupitia jukwaa hilo.
Hata hivyo, jukwaa hilo linatarajia kuanzisha tuzo mbalimbali za MWANAMKE MJASILIAMALI kwa wilaya ya Kahama, ikiwalenga wanawake wajasilimali katika kuwainua.
