Kahama FM

Sheria na kanuni za matumizi ya barabara yazingatiwe

August 19, 2025, 12:26 pm

Mrakibu wa Polisi na Mkuu wa Usalama Barabarani wilayani Kahama Flora Nangawe (Picha na John Juma)

”watembea kwa miguu zingatieni upande wao sahihi wa kupita, kwa mjibu wa sheria za usalama barabarani ni mkono wa kulia wa mtumiaji ili kutoa nafasi ya kuona chombo cha moto kilichombele yake”

Na John Juma

Watumiaji wa barabara katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali zisizo za lazima pamoja na kuondokana na adhabu.

Hayo yamesemwa na Mrakibu wa Polisi na Mkuu wa Usalama Barabarani wilayani Kahama Flora Nangawe wakati akizungumza na Kahama fm ofisini kwake, ambapo amesema madereva na watembea kwa miguu wanapswa kuzifahamu sheria za usalama barabarani kwa usalama wao.

Nangawe amewataka watembea kwa miguu kuzingatia upande wao sahihi wa kupita ambao kwa mjibu wa sheria za usalama barabarani ni mkono wa kulia wa mtumiaji ili kutoa nafasi ya kuona chombo cha moto kilichombele yake.

Sauti ya Mrakibu wa Polisi na Mkuu wa Usalama Barabarani wilayani Kahama Flora Nangawe

Nao, Watumiaji wa barabara wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti akiwemo, Marium Emmanuel, Remidius Kaijage na Malaki Firmoni wamezitaka mamlaka kuweza kuborehsa miundo mbinu pamoja na kutoa elimu juu ya usalama barabarani.

Sauti za watumiaji wa barabara katika Manispaa ya Kahama

Kwa upande wao madereva wa vyombo vya moto akiwemo Yossam Abdallah na Krivin James wameiomba serikali kuboresha miundombinu ili kuwe na njia ya watembea kwa miguu ili kuondokana na ajali za mara kwa mara.

Sauti za madereva wa vyombo vya moto akiwemo Yossam Abdallah na Krivin James

Barabara ni moja kati ya miundombinu muhimu inayokuza uchumi wa nchi yetu na kuchangia ukuaji wa Taifa kwa kiasi kikubwa kwa kupanua biashara ya ndani na kimataifa kwa njia ya usafirishaji.