Kahama FM

Viongozi Kahama watakiwa kusikiliza, kutatua kero za wananchi

July 10, 2025, 5:17 pm

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita na na mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda wakiwa katika tukio la makabidhiano ya ofisi (Picha na Sebastian Mnakaya)

”kasikilizeni na kuzitatua changamoto mbalimbali za wananchi wenu pamoja na kushirikiana katika suala ya maendeleo” Mboni Mhita

Na Sebastian Mnakaya

Viongozi wa wilayani ya Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kuendelea kusikiliza na kutatua changamoto mbali mbali za wananchi wao pamoja na ukamilishaji wa miradi ya maendeleo.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita wakati wa hafla ya kukabidhiana ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda, ambapo amemtaka kushirikiana na wananchi katika shughuli za maendeleo, huku wakikamilisha miradi hiyo kwa mapato ya ndani.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita

Kwa upande wake mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Kahama Thomasi Muyonga, amemtaka mkuu wa wilaya huyo, Frank Nkinda kuendelea kutekeleza shughuli za kimaendeleo baada mtangulizi wake kuwa mkuu mkoa wa Shinyanga.

Sauti mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Kahama Thomasi Muyonga
Mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda

Nae, mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda wakati akikabidhiwa ofisi hiyo, amesema kuwa amepokea maagizo hayo na atayasimamai vyema kwa kushirikiana na wananchi katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda

Wilaya ya Kahama ina jumla ya halmashauri tatu akiwemo Manispaa ya Kaham, Halmashauri ya Ushetu na Msalala, ikiwa na jumla ya mitaa 35, vijiji 146 na vitongoji 1,150.